728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 17, 2015

    MAKUBWA:STRAIKA IRAN AKOSA MICHUANO KISA MUME KUNG'ANG'ANIA PASSPORT

    Iran

    Hali ya mambo nchini Iran bado ni tete kwa watu wenye jinsia ya kike.Mbali ya wanawake nchini Iran kuzuiliwa kufanya mambo mengi binafsi lakini hata katika yale yenye maslahi kwa taifa bado wameendelea kuzuiliwa kuyafanya.

    Taarifa zilizoifikia Soka Extra kutoka Iran zinasema kuwa nahodha wa timu ya taifa hilo ya wanawake Ardalan hatakwenda na timu hiyo katika michuano ya soka itakayofanyika huko Malysia baada ya mumewe kukataa kusaini nyaraka zitakazo msaidia aweze kupata hati mpya ya kusafiria (passport) kwani iliyopo imekwisha muda wake.
    Niloufar Ardalan and the rest of the Iranian women's team at a 2012 tournament
    Ardalan,30 maarufu kwa jina la Lady Goal amesema mume wake ambaye ni mwandishi wa habari bwana Mehdi Toutounchi amekataa kusaini nyaraka hizo hivyo hatoweza kusafiri na timu kuelekea Malysia katika michuano ya Asian Football Federation Women's Futsal Championship

    "Mume wangu amekataa kusaini nyaraka hizo hivyo siwezi kusafiri.Nadhani serikali ingekuja na suluhisho na kutoa nafasi kwa wanawake kujitetea katika masuala kama haya.Kama mwanamke wa Kiislam nilitaka kuipeperusha vyema bendera ya taifa langu badala ya kusafiri tu kwa starehe na mambo mengine."

    Serikali nchini Iran imewapa nguvu wanaume dhidi ya wanawake kwani ili mwanamke aweze kusafiri ni lazima mume akubali.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAKUBWA:STRAIKA IRAN AKOSA MICHUANO KISA MUME KUNG'ANG'ANIA PASSPORT Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top