728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, September 27, 2015

    MASIKINI JUVENTUS YAENDELEA KUWA KIBONDE ITALIA,YAGONGWA NA NAPOLI,IMEVUNA POINTI TANO TU KATIKA MECHI SITA

    Napoli,Italia.

    Juventus imeendelea kuwanyong'onyesha mashabiki wake baada ya usiku wa kuamkia leo kukubali kichapo cha mabao 2-1 toka kwa Napoli katika muendelezo wa michezo ya Seria A.

    Juventus iliyokuwa mgeni Katika dimba la Estadio San Paolo ilionyesha mapema kuushindwa muziki wa Napoli baada ya kuwa nyuma kwa magoli mawili ya Lorenzo Insigne na Gonzalo Higuain kabla ya kujipatia goli la kujifutia machozi kupitia kwa kiungo Mario Lemina.

    Kufuatia kichapo hicho Juventus huenda ikajikuta katika inashika nafasi ya 13 katika msimamo wa Seria A ikiwa vinara Inter Milan wataifunga Fiorentina leo jumapili.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MASIKINI JUVENTUS YAENDELEA KUWA KIBONDE ITALIA,YAGONGWA NA NAPOLI,IMEVUNA POINTI TANO TU KATIKA MECHI SITA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top