728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 26, 2015

    SPEED 160:YANGA YAIFUMUA SIMBA 2-0 U/TAIFA,TAMBWE,BUSUNGU WAPELEKA KILIO MSIMBAZI,KIIZA AZIMWA

    Dar es salaam,Tanzania.

    Yanga FC imeendelea kujichimbia kileleni mwa ligi kuu Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Simba SC katika mchezo mkali na uliojaa ubabe uliopigwa jioni ya leo katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

    Magoli ya Yanga yaliyopeleka simanzi Msimbazi yamefungwa na Hamis Tambwe kwa shuti kali la mguu wa kushoto katika dakika ya 44 ya kipindi cha kwanza huku lile la pili likifungwa kwa kichwa na Malimi Busungu dakika ya 80 akiunganisha vyema mpira wa kurushwa wa mlinzi Mbuyu Twite ambaye baadae alilimwa kadi nyekundu kwa mchezo mbaya.

    Matokeo mengine ligi kuu bara

    JKT Ruvu 0-1 Stand United (Elias Maguli)
    Coastal Union 0-0 Mwadui FC
    Mtibwa 0-0 Majimaji
    Prisons 1-0 Mgambo FC

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SPEED 160:YANGA YAIFUMUA SIMBA 2-0 U/TAIFA,TAMBWE,BUSUNGU WAPELEKA KILIO MSIMBAZI,KIIZA AZIMWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top