728x90 AdSpace

  • Latest News

      Sunday, September 27, 2015

      EL MERREIKH YAIZIMA TP MAZEMBE 2-1NUSU FAINALI AFRIKA,ULIMWENGU ATUPIA AKITOKEA BENCHI

      Merreikh,Sudan.

      Magoli mawili ya Bakri Babeker na Francis Coffie yameiwezesha El Merreikh Kuibuka na ushindi wa magoli 2-1dhidi ya TP Mazembe katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya ligi ya mabingwa Afrika uliopigwa jana jumamosi huko Sudan.

      El Merreikh ilijipatia magoli hayo dakika za 44 na 80 huku lile la kufutia machozi la TP Mazembe likifungwa na Mtanzania Thomas Ulimwengu dakika ya 77 aliyekuwa ameingia akitokea benchi.

      Mchezo wa pili wa nusu fainali ya ligi hiyo kubwa Afrika utachezwa wiki ijayo huko Congo na mshindi atatinga katika fainali.





      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: EL MERREIKH YAIZIMA TP MAZEMBE 2-1NUSU FAINALI AFRIKA,ULIMWENGU ATUPIA AKITOKEA BENCHI Rating: 5 Reviewed By: Unknown