728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, March 15, 2017

    Emmanuel Okwi aendeleza U-Samatta ligi kuu Uganda.

    Kampala,Uganda.

    Emmanuel Okwi ameendelea kupachika mabao matamu kwenye michezo ya ligi kuu ya Uganda kama ilivyo kwa Mtanzania Mbwana Samatta anayetesa kwasasa nchini Ubelgiji akiwa na KRC Genk hii ni baada ya jana Jumanne kufunga bao moja na kuiwezesha SC Villa kuichapa The Saints mabao 2-0 katika mchezo mgumu uliochezwa kwenye uwanja uliojaa tope kutokana na mvua kubwa kunyesha huko Mwerwere.

    Okwi ambaye amerejea Uganda hivi karibuni na kujiunga na SC Villa akiwa kama mchezaji baada ya mambo kumwendea kombo nchini Denmark,amefunga bao hilo kwa mkwaju mkali wa mbali katika dakika ya 64 ya mchezo na kufikisha mabao saba katika michezo saba.Bao la pili la SC Villa limefungwa na mlinzi wake wa kati,John Adriko. 

    Ikumbukwe Jumapili iliyopita Okwi aliibuka tena shujaa baada ya kuifungia SC Villa mabao matatu katika ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Onduparaka FC.

    Matokeo ya michezo mingine ya Jana Jumanne

    Express 4-3 Police
    The Saints 0-2 SC Villa
    Soana 1-1 JMC Hippos
    BUL 2-0 Bright Stars
    Sadolin 0-0 Lweza



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Emmanuel Okwi aendeleza U-Samatta ligi kuu Uganda. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top