728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, March 19, 2017

    TP Mazembe yatupwa nje ligi ya mabingwa Afrika

    Harare,Zimbabwe.

    TP Mazembe Englebert imetupwa nje ya michuano ya klabu bingwa Afrika na kujikuta ikiangukia kwenye michuano ya shirikisho baada ya jioni ya leo kulazimishwa sare ya bila kufungana na mabingwa wa Zimbabwe,Caps United katika mchezo mkali wa marudiano wa hatua ya mtoano uliochezwa katika uwanja wa taifa wa Zimbabwe uliopo jijini Harare.

    Ikumbukwe katika mchezo wa awali uliochezwa Jumapili iliyopita huko Lubumbashi,DR Congo timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1.Caps United walipata bao kupitia kwa Abbas Amidu wakati bao la wenyeji TP Mazembe lilifungwa na nahodha wake,Rainford Kalaba.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TP Mazembe yatupwa nje ligi ya mabingwa Afrika Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top