728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, May 14, 2016

    TIMU YA WANAWAKE YA ARSENAL YATWAA UBINGWA WA FA BAADA YA KUICHAPA CHELSEA KATIKA FAINALI

    London,England.

    Timu ya Wanawake ya Arsenal jioni ya leo imetwaa ubingwa wa kombe la FA baada ya kuichapa timu ya Wanawake ya Chelsea kwa bao 1-0 katika mchezo mkali wa fainali uliopigwa katika uwanja wa Wembley jijini London.

    Bao pekee la mchezo huo uliopigwa mbele ya watazamani 32,912 limefungwa dakika ya 18 ya kipindi cha kwanza na mshambuliaji kinda Danielle Carter.

    Kabla ya kufunga bao hilo Carter,22 alimlamba chenga Hannah Blundell kabla ya kufumua mkwaju mkali uliomshinda mlinda mlango wa Chelsea Hedvig Lindahl na kutinga wavuni na kuifanya Arsenal itwae ubingwa wa 14 wa kombe hilo kongwe zaidi England.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TIMU YA WANAWAKE YA ARSENAL YATWAA UBINGWA WA FA BAADA YA KUICHAPA CHELSEA KATIKA FAINALI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top