728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, May 27, 2016

    WACHEZAJI AZAM FC WAPEWA LIKIZO YA WIKI TANO

    Dar es Salaam,Tanzania

    WACHEZAJI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC,wamepewa mapumziko ya wiki tano baada ya kumaliza mechi ya mwisho
    ya msimu wa 2015/16 dhidi ya Yanga kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la
    Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) juzi jioni.

    Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba, alisema kuwa msimu ndio umeisha kwa timu hiyo na kilichobakia ni kujipanga kwa ajili ya kupata matokeo mazuri msimu ujao.

    “Tunamshukuru Mwenyezi Mungu tumecheza mchezo wa fainali, ingawa matokeo yalikuwa si mazuri haikuwa
    malengo yetu, tulipanga kushinda lakini lazima tukubali ni matokeo ya mpira,” alisema.

    Kawemba alisema wachezaji watamaliza likizo hiyo Juni 30 mwaka huu na Julai Mosi wataanza maandalizi ya msimu mpya.

    “Kwa hiyo tutafanya nini kwa msimu ujao,tutamuongeza nani, tutamtoa nani hayo tutazungumza baadaye
    lakini sasa hivi tunawaomba washabiki wetu wawe watulivu na
    tutaendelea kujipanga,” alisema.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WACHEZAJI AZAM FC WAPEWA LIKIZO YA WIKI TANO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top