728x90 AdSpace

Sunday, May 22, 2016

MAPYA YAIBUKA KATI YA MAN UNITED NA ZLATAN IBRAHIMOVIC

Sweden.

IBRAHIMOVIC kuwa kocha msaidizi Manchester United.Zlatan Ibrahimovic ameshatangaza kuwa anaondoka Paris Saint-Germain pasipo kusema ni wapi ataelekea.

Lakini habari zilizoifikia Soka Extra hizi punde kutoka mtandao wa Goal.Com ni kuwa Zlatan Ibrahimovic anaelekea Manchester United.

Ndiyo Manchester United tena kuwa kocha msaidizi na siyo mchezaji.

Kwa mujibu wa chombo kimoja cha habari cha Swedeni kinachoitwa Aftonbladet ni kuwa mshambuliaji huyo mwenye miaka 34 anakwenda Manchester United kuwa msaidizi wa Kocha Jose Mourinho na siyo kama mchezaji.

Je,kweli?Tusubiri tuone......!!Mpira una mambo mengi sana!!


  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: MAPYA YAIBUKA KATI YA MAN UNITED NA ZLATAN IBRAHIMOVIC Rating: 5 Reviewed By: Unknown