728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, May 28, 2016

    RASHFORD AENDELEA KUFANYA MAAJABU,AVUNJA REKODI YA MWAKA 1938

    Sunderland, England.

    Marcus Rashford ameweka rekodi ya kuwa mchezaji mdogo zaidi kuwahi kuifungia bao England katika mchezo wake wa kwanza (debut) wa kikosi cha wakubwa baada ya Ijumaa usiku kufunga bao moja na kuiwezesha England kutoka uwanjani kifua mbele kwa ushindi wa mabao 2-1dhidi ya Australia katika mchezo wa Kimataifa wa kirafiki uliochezwa huko Sunderland katika uwanja wa Stadium of Light.

    Rashford akiwa na umri wa miaka 18 na siku 208 amefunga bao hilo dakika ya tatu tu ya machezo kwa mkwaju mkali akiunganisha krosi ya winga Raheem
    Sterling na kumuacha mlinda mlango wa Australia Mathew Ryan akichupa bila mafanikio.

    Bao jingine la England katika mchezo huo limefungwa na nahodha Wayne Rooney dakika ya 55 huku lile la Australia likipatikana baada ya kiungo wa England Erik Dier kujifunga akiwa katika harakati za kuokoa.

    Kufuatia bao hilo Rashford  amefanikiwa kuivunja rekodi iliyowekwa Octoba,22,1938 na mshambuliaji wa zamani wa vilabu vya Everton,Chelsea na Arsenal Tommy Lawton.

    Lawton akiwa na umri wa miaka 19 na siku 318 aliifungia England bao katika mchezo wake wa kwanza.Katika huo uliochezwa katika uwanja wa Ninian Park,England ilifungwa mabao 4–2 na ndugu zao Wales.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RASHFORD AENDELEA KUFANYA MAAJABU,AVUNJA REKODI YA MWAKA 1938 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top