728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, March 21, 2017

    Antoine Griezmann bado hasomeki kabisa


    Madrid,Hispania.

    Antoine Griezmann amesema kwamba ana furaha katika klabu yake ya Atletico Madrid na amesisitiza kwamba mustakabali wake upo mikononi mwa klabu.

    Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ameripotiwa kuwindwa na klabu ya Manchester United.

    Griezmann alisema jana," Nimeshasema sana hapo nyuma, nina mkataba na Atletico Madrid na nina furaha hapa pamoja na Familia yangu."

    "Na hata hivyo, kuondoka hapa, itatakiwa klabu itake kuniuza mimi au sio ? "

    "Najaribu kuwa na furaha nikiwa uwanjani na kuisaidia klabu kupata matokeo. kila kitu kinaenda sawa. Hapa jua linatoka mwaka mzima na hiyo pia inasaidia."

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Antoine Griezmann bado hasomeki kabisa Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top