728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, May 04, 2016

    UCHAGUZI MKUU YANGA SC WASOGEZWA MBELE,KISA?

    Dar es salaam,Tanzania.

    Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imetangaza Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga kuwa utafanyika Juni 25,2016 badala ya Juni 5,2016.

    Kamati ya Uchaguzi ya TFF imelazimika kufanya hivyo kwa kuzingatia ushiriki wa
    Yanga ambayo inashiriki michuano ya kimataifa.

    Sekretarieti ya Yanga ambayo ingefanya kazi kwa pamoja na Kamati ya Uchaguzi kwa kushirikiana na TFF kwa sasa inashughulikia pia kuiandaa timu kwa ajili ya michuano ya kimataifa.

    Yanga inatarajiwa kucheza na Esperanca ya Angola katika michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika Mei 7, mwaka huu kabla ya kurudiana kati ya Mei 17 na 18,mwaka huu huko Angola.

    Kwa mujibu wa ratiba mpya, fomu za kuwania uongozi wa Yanga zitaanza
    kuchukuliwa Mei 25, 2016 na kwamba uchaguzi huo utafanyika ndani ya muda
    ambao Serikali kwa kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) iliagiza uchaguzi kufanyika kabla ya Juni 26, 2016 hivyo uchaguzi utafanyika ndani ya wakati.

    Katiba itakayotumika ni ya mwaka 2010 na kwamba Wanachama wa Yanga watatumia kadi za kawaida za uanachama na si za benki.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: UCHAGUZI MKUU YANGA SC WASOGEZWA MBELE,KISA? Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top