Tenerife,Hispania.
WINGA wa kimataifa wa Tanzania,anayekipiga Azam FC Farid Mussa Malik amefuzu majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Deportivo Tenerife ya Ligi Daraja la pili nchini Hispania maarufu kama Segunda B.
Habari hiyo njema kwa soka la Tanzania imeripotiwa na Mkurugenzi wa Azam FC, Yussuf Bakhresa anayefuatilia majaribio ya mchezaji huyo huko Hispania,.
Kilichobaki sasa ni vilabu vya CD Tenerife na Azam FC kukaa mezani na kufanya mazungumzo juu ya kuuziana mchezaji huyo anayekipiga pia Taifa Stars.
0 comments:
Post a Comment