728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 02, 2015

    WAMEMNASA:CHELSEA KUMSAINISHA LEO KIPA ALIYETWAA KOMBE LA DUNIA

    London,England.

    Chelsea imeripotiwa kufanikiwa kushinda mbio za kumsajili kipa mkongwe Marco Amelia toka Italia aliyekuwa pia akipigiwa hesabu na Arsenal.

    Amelia anatarajiwa kusaini kuichezea Chelsea leo ijumaa kwa mkataba wa msimu mmoja baada ya kufaulu majaribio aliyofanya wiki iliyopita.Chelsea iliamua kumgeukia Amelia aliyekuwa huru baada ya kipa wake namba moja Thibaut Courtois kufanyiwa upasuaji kufuatia kupata jeraha la goti mwanzoni mwa msimu huu.

    Amelia,33 ameshacheza michezo 317 akiwa na vilabu vya Livorno, Palermo, Genoa na AC Milan huku mwaka 2006 akiwa katika kikosi cha Italia kilichotwaa kombe la dunia nchini Ujerumani wakati huo kikiwa chini ya kocha Marcello Lippi.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAMEMNASA:CHELSEA KUMSAINISHA LEO KIPA ALIYETWAA KOMBE LA DUNIA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top