728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 14, 2015

    REAL MADRID YAMTAKA SANCHEZ,KUTOA MTONYO NA MCHEZAJI

    Madrid,Hispania.

    Gazeti la michezo la Don Balon la Hispania limekuja na habari ambayo siyo nzuri sana kwa mashabiki wa Arsenal duniani kote.

    Don Balon limeripoti kuwa Real Madrid inaandaa kitita cha £37.3m pamoja na winga Denis Cheryshev ili kumsajili staa wa Arsenal Mchile Alexis Sanchez (26) aliyewahi pia kukipiga na FC Barcelona.

    Real Madrid imeamua kumjumuisha Cheryshev mwenye thamani ya £15m katika dili hilo kutokana na winga huyo raia wa Urusi kuwa ni kipenzi kikubwa cha kocha wa Arsenal Mfaransa Arsene Wenger.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: REAL MADRID YAMTAKA SANCHEZ,KUTOA MTONYO NA MCHEZAJI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top