728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 14, 2015

    ANAKUJA:ANCELOTTI,BAYERN KIMEELEWEKA

    Milan,Italia.

    Muitaliano Carlo Ancelotti ndiye atakayerithi mikoba ya Pep Guardiola katika klabu ya Bayern Munich msimu ujao hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Sport Mediaset wa Italia.

    Sport Mediaset imeongeza kuwa Ancelotti na Bayern Munich tayari wameshafanya makubaliano ya awali na kocha huyo wa zamani wa vilabu vya AC Milan,Chelsea,PSG na Real Madrid amekubali kusaini mkataba wa miaka miwili ili kuziba nafasi ya Guardiola anayesemekana kutimkia Manchester City pindi mkataba wake utakapoisha mwishoni mwa msimu huu.

    Ancelotti ambaye alikuwa akifukuziwa na klabu ya Liverpool ili kuchukua nafasi ya Brendan Rodgers kabla ya kudengua amekuwa hana timu tangu alipotimuliwa na Real Madrid msimu uliopita.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ANAKUJA:ANCELOTTI,BAYERN KIMEELEWEKA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top