728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, June 14, 2016

    DUNGA ATUPIWA VIRAGO BRAZIL

    Sao Paulo,Brazil.

    CHAMA cha soka cha Brazil (CBF) kimetangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha wake mkuu wa timu yake ya taifa Carlos Caetano Bledorn
    Verri Dunga 

    Dunga,52,mshindi wa kombe la dunia la mwaka 1994 nchini Marekani ameondolewa katika wadhifa huo baada ya Jumatatu alfajiri Brazil kutupwa nje ya michuano ya Copa America Centenario kufuatia kukubali kichapo cha bao 1-0 toka kwa Peru.

    Mbali ya Dunga,aliyekuwa msaidizi wake,Gilmar Rinaldi na wengine pia nao wametupiwa virago.

    Hii ni mara ya pili kwa Dunga kukumbwa na kadhia hiyo mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 2010 baada ya Brazil kuondolewa katika hatua ya makundi ya kombe la dunia lililofanyika Afrika Kusini.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: DUNGA ATUPIWA VIRAGO BRAZIL Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top