728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, June 25, 2016

    VITUKO VYA EURO 2016:IKER CASILLAS AMCHAPA KOFI PIQUE MAZOEZINI KISA KUPIGWA TOBO

    Nice,Ufaransa.

    KATIKA hali isiyotarajiwa Mlinzi wa Hispania,Gerard Pique amejikuta akichapwa Kofi kali la shavuni na Iker Casillas kufuatia kumkosakosa kumpiga tobo kipa huyo wa zamani wa Real Madrid.

    Tukio hilo limetokea Jana Ijumaa wakati wachezaji wa Hispania/La Roja walipokuwa wakifanya mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wao wa hatua ya 16 bora dhidi ya Italia.

    Japo Casillas alifaulu kukwepa fedheha ya kupigwa tobo hilo kwa kuwahi kubana miguu yake lakini jaribio hilo la Pique lilionekana kumkera Kipa huyo mkongwe na kuamua kujibu mapigo kwa kurusha kofi kali lililompata sawia Pique na kumfanya ahamaki na kutaka kulipiza lakini wachezaji wenzao waliingia kati na kutuliza hali ya mambo.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: VITUKO VYA EURO 2016:IKER CASILLAS AMCHAPA KOFI PIQUE MAZOEZINI KISA KUPIGWA TOBO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top