728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, June 22, 2016

    KAVUMBAGU:LIGI YA BONGO YATAKA MOYO



    STRAIKA wa kimataifa aliyemaliza mkataba Azam FC, Didier Kavumbagu, amenyoosha mikono na kueleza wazi kwamba wachezaji kutoka nje ya nchi wanaokuja kucheza soka Tanzania, wanatakiwa kuwa na moyo wa chuma.

    Akizungumza jana, Kavumbagu alisema wachezaji kutoka nchini Burundi ni miongoni mwa wahanga ambao wameshindwa kufanya vizuri katika baadhi ya klabu ikiwemo Simba.

    Wachezaji waliotoka nchini humo na kushindwa kucheza kwa muda mrefu ni Gilbert Kaze, Pierre Kwizera na Kelvin Ndayisenga ambao walishindwa kufanya vizuri kisha kutimka.

    “Ligi ya Tanzania ni  tofauti na Burundi,  ni lazima kuwa na moyo mgumu vinginevyo huwezi kufanya kazi kwani kuna matatizo makubwa ndani na nje ya uwanja yanasumbua ambayo yamekuwa ni kikwazo kwa wachezaji wengi kutofanikiwa,” alisema.

    Kavumbagu amemaliza mkataba na timu hiyo ambapo kwa sasa yupo nchini Burundi kusikilizia ofa kutoka timu za Mbeya City ya Tanzania, Qatar na nchini Vietnam.

    CHANZO:DIMBA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KAVUMBAGU:LIGI YA BONGO YATAKA MOYO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top