728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, June 30, 2016

    ULIMWENGU:HUYU CHIRWA BADO SANA ILA MAHADHI SAFI

    Dar es Salaam,Tanzania.

    MSHAMBULIAJI Mtanzania  anayecheza katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Thomas Ulimwengu, amesema kiwango kilichoonyeshwa na Mzambia,  Obrey Chirwa wa Yanga ni cha kawaida sana.

    Chirwa amesajiliwa Yanga katika kipindi cha dirisha dogo la usajili katika michuano ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) akitokea Platnum ya Zimbabwe.

    Mchezaji huyo alikuwa katika kikosi cha Yanga kilichocheza juzi na TP Mazembe kwenye Uwanja wa  Taifa jijini Dar es Salaam ambao walifungwa bao 1-0.

    Akimzungumzia Chirwa, Ulimwengu   alisema kiwango kilichoonyesha na mchezaji huyo ni cha kawaida na anatakiwa kupewa muda ili aweze kuonyesha uwezo wake.

    Ulimwengu alisema Chirwa anahitaji muda kwani anaonekana hajawa fiti kucheza soka la Tanzania.
    “Chirwa anaonekana mgeni, halijui soka la Tanzania wala viwanja vyake tofauti na Mahadhi ambaye Uwanja wa Taifa si mara ya kwanza kucheza,” alisema Ulimwengu.

    Ulimwengu alisema mchezaji huyo si mbaya, lakini anaonekana bado mgeni kutokana na mazingira ila akiendelea kucheza anaweza kuwa  tishio.

    CHANZO:BINGWA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ULIMWENGU:HUYU CHIRWA BADO SANA ILA MAHADHI SAFI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top