728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, June 28, 2016

    CHILE YATAWALA KIKOSI BORA CHA COPA AMERICA,YAINGIZA WACHEZAJI WANANE

    Mchezaji bora wa Copa America:Alexis Sánchez

    New Jersey,Marekani.

    SHIRIKISHO la Soka la Amerika Kusini CONMEBOL limetoa majina ya wachezaji XI waliofanya vizuri katika michuano ya Copa America Centenario iliyofikia tamati yake Alfajiri ya jana Jumatatu na Chile kuibuka Mabingwa kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuwafunga Argentina kwa penati 4-2 katika mchezo mkali wa Finali uliochezwa katika uwanja wa MetLife huko New Jersey,Marekani.

    Katika kikosi hicho Mabingwa Chile wameingiza wachezaji wanane ambao ni Claudio Bravo,Mauricio Isla, Gary Medel na Jean Beausejour.

    Wengine ni Arturo Vidal,Charles Aranguiz,Alexis Sánchez na Eduardo Vargas.

    Argentina wao wameingiza wachezaji watatu ambao ni Nicolás Otamendi ,Javier Mascherano na Lionel Messi.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHILE YATAWALA KIKOSI BORA CHA COPA AMERICA,YAINGIZA WACHEZAJI WANANE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top