728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, June 23, 2016

    TFF KUINGIA KATI ISHU YA KESSY

    Dar es Salaam,Tanzania.

    SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF), linatarajia kuwaweka meza moja vigogo wa Simba na Yanga ili kumaliza sakata la usajili na kibali cha Hassan Ramadhan ‘Kessy’.

    Hatua hiyo imekuja baada ya Yanga kuwasilisha nakala ya barua ikiwa imeambatanishwa na mkataba wa Kessy na Simba ambao unaonyesha wazi kuwa ulimalizika Juni 15, mwaka huu na mchezaji huyo alikuwa sahihi kuingia mkataba mpya na klabu nyingine.

    Yanga ilishindwa kumtumia Kessy katika mchezo wake wa kwanza wa Kundi A, Kombe la Shirikisho Afrika wakifungwa 1-0 na Mo Bejaia nchini Algeria baada ya CAF kuomba barua ya kuruhusiwa kwake kuondoka klabu yake ya zamani, Simba ambayo hawakuwa nayo.

    Akizungumza, Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas, alisema kuwa iwapo Simba hawatajibu barua hiyo waliyoandikiwa na wapinzani wao basi watalazimika kuita viongozi wa pande zote mbili na kukaa nao meza moja.

    “Yanga wamepeleka barua Simba ambayo nakala imeletwa TFF na CAF (Shirikisho la Soka Afrika) hivyo tunasubiri majibu ya Simba wasipojibu kwa wakati tutawasiliana na pande zote mbili,” alisema.
    Katika barua hiyo ya Yanga imeiomba TFF iwasaidie kumwidhinisha beki huyo kuanza kazi Jangwani ikiwa hadi kesho (Ijumaa) Simba watakuwa hawajajibu barua hiyo.

    Yanga inaamini kuwa kama klabu ya zamani ya Kessy, Simba itagoma kujibu barua hiyo itakuwa imemaanisha kuwa haina pingamizi kwa staa huyo kuichezea miamba hiyo Jangwani.

    Na iwapo Simba SC watamwekea pingamizi Kessy, watapaswa kuwa na hoja za pingamizi ambalo litasikilizwa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF chini ya Mwenyekiti wake, Wakili Richard Sinamtwa.

    CHANZO:BINGWA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TFF KUINGIA KATI ISHU YA KESSY Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top