728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, June 25, 2016

    KUZIONA YANGA,TP MAZEMBE SHIRIKISHO VIINGILIO HIVI HAPA

    Dar es Salaam,Tanzania.

    YANGA SC imetangaza viingilio vitakavyotumika kushuhudia mchezo
    wake wa Kundi A wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe ya Congo DRC unaotarajiwa kuchezwa Jumanne katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

    Akiongea na waandishi wa Habari makao makuu ya klabu, Jangwani, jijini Dar es Salaam leo,Mkuu wa Idara ya habari na Mawasiliano ya Yanga,
    Jerry Muro amesema Yanga imepanga viingilio viwili pekee ambavyo ni Sh. 7000 kwa majukwaa ya
    mzunguko na Sh. 30,000 kwa jukwaa Maalumu (VIP).

    Aidha mkuu huyo ameongeza kuwa tiketi za mtanange huo unaosubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka nchini zitaanza kuuzwa siku ya Jumatatu.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KUZIONA YANGA,TP MAZEMBE SHIRIKISHO VIINGILIO HIVI HAPA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top