728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, June 23, 2016

    EURO 2016:UBELGIJI YAIFUMUA SWEDEN NA KUFUZU 16 BORA,ITALIA CHALI KWA IRELAND

    Nice,Ufaransa.

    UBELGIJI imeungana na Italia pamoja na Jamhuri ya Ireland kufuzu hatua ya 16 bora kutoka kundi E baada ya Jumatano usiku kuifunga Sweden kwa bao 1-0 katika mchezo wa mwisho wa makundi uliochezwa katika uwanja wa Allianz Riviera mjini Nice.

    Bao pekee la mchezo huo uliokuwa wa mwisho kwa mshambuliaji wa Sweden Zlatan Ibrahimovic anayestaafu limefungwa dakika ya 84 kwa mkwaju mkali na Kiungo Rajda Nainggolan baada ya kupokea pasi safi ya nahodha Eden Hazard toka wingi ya kushoto.

    VIKOSI

    Sweden : Isaksson, Johansson, Granqvist,Olsson, Forsberg, Ekdal, Kallstrom,Ibrahimovic, Berg, Lindelof

    Belgium: Courtois, Meunier,
    Alderweireld, Vermaelen, Vertonghen,Witsel, Nainggolan, De Bruyne, Carrasco,Hazard, Lukaku

    Katika mchezo mwingine wa kundi E uliochezwa katika uwanja wa Stade Pierre Mauroy,bao la dakika ya 85 la Robbie Brady limeipa Jamhuri ya Ireland ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Italia.

    Kwa matokeo hayo Italia,Ubelgiji na Jamhuri ya Ireland zimefanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora huku Sweden ikitupwa nje baada ya kuambulia alama moja katika michezo mitatu.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: EURO 2016:UBELGIJI YAIFUMUA SWEDEN NA KUFUZU 16 BORA,ITALIA CHALI KWA IRELAND Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top