728x90 AdSpace

  • Latest News

      Saturday, June 03, 2017

      Klabu bingwa Afrika:Mamelodi Sundowns yalala nyumbani


      Pretoria,Afrika Kusini.

      YASSINE Khensissi akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga mabao mawili na kuiwezesha Esperance du Tunis ya Tunisia kuwafunga mabingwa watetezi Mamelodi Sundowns mabao 2-1 katika mchezo wa kundi C wa michuano ya klabu bingwa Afrika uliochezwa kwenye uwanja wa  Lucas Moripe,Pretoria-Afrika Kusini.

      Bao la kufutia machozi la Mamelodi Sundowns limefungwa na Sibusiso Vilakazi.Ushindi huo umeifanya Esperance du Tunis ikae kileleni mwa msimamo wa kundi C baada ya kufikisha pointi 7.Pointi 3 mbele ya Mamelodi Sundowns inayoshika nafasi ya pili na pointi zake 4.


      Mchezo mwingine wa kundi C utachezwa kesho Jumapili ambapo AS Vita Club ya DR Congo itasafiri kwenda Addis Ababa,Ethiopia kuvaana na St. George.

      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: Klabu bingwa Afrika:Mamelodi Sundowns yalala nyumbani Rating: 5 Reviewed By: Unknown