728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, June 23, 2017

    MONACO YASALIMU AMRI YAKUBALI KUMWACHIA TIEMOUE BAKAYOKO


    Monaco,Ufaransa.

    MONACO imesalimu amri mbele ya noti za matajiri wa Chelsea baada ya kukubali kumuuza kiungo wake mkabaji, Tiemoue Bakayoko kwa dau la £35.2m.

    Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya vilabu hivyo kuwa kwenye mazungumzo ya kipindi kirefu ya kutaka kuuziana kiungo huyo mwenye umri wa miaka 22.

    Msimu uliopita Bakayoko alifanikiwa kuvitoa udenda vilabu vingi vikubwa baada ya kuonyesha kiwango cha juu cha usakataji kabumbu kilichoiwezesha Monaco kutwaa ubingwa wake wa kwanza wa Ligue 1 pamoja na kufika nusu fainali ya michuano ya klabu bingwa Ulaya.

    Kusajiliwa kwa Bakayoko kumedaiwa huenda kukafungua milango kwa kiungo,Nemanja Matic anayehusishwa na mpango wa kutaka kuhamia Manchester United kwenda kuungana na kocha wake wa zamani José Mourinho.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MONACO YASALIMU AMRI YAKUBALI KUMWACHIA TIEMOUE BAKAYOKO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top