728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, June 23, 2017

    MOHAMMED SALAH ATUA LIVERPOOL KWA BILIONI 8.5


    Liverpool,England.

    KLABU ya Liverpool imekamilisha usajili wa winga wa zamani wa Chelsea, Mohammed Salah kutoka AS Roma ya Italia kwa ada ya uhamisho ya £34.4m (Bilioni 8.5).

    Salah,25,anayetokea Misri amesaini mkataba wa miaka mitano na kukabidhiwa jezi namba 11 ambayo awali ilikuwa inavaliwa na Roberto Firmino aliyepewa jezi namba 9.

    Salah aliyekubali mshahara wa £90,000 kwa wiki anakuwa mchezaji wa pili kujiunga na Liverpool katika kipindi hiki cha usajili barani Ulaya.Mwingine ni Dominic Solanke aliyetokea Chelsea.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MOHAMMED SALAH ATUA LIVERPOOL KWA BILIONI 8.5 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top