728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, May 18, 2017

    AS Monaco yatwaa ubingwa wa Ligue 1 baada ya miaka 17



    Paris,Ufaransa.

    WACHEZAJI wa AS Monaco wakishangilia baada ya usiku huu kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa Ligue 1 kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2000,miaka 17 iliyopita hii ni kufuatia ushindi wao wa mabao 2-0 nyumbani Stade Louis II dhidi ya wageni wao Saint-Etienne.
    Kylian Mbappe (left) celebrates with Radamel Falcao after breaking the deadlock
    Mchezaji bora chipukizi wa mwaka,Kylian Mbappe aliiandikia AS Monaco bao la kwanza katika dakika ya 19 kabla ya Valere Germain kufunga la pili katika dakika ya 93 na kuipa miamba hiyo ubingwa wake wa nane wa Ligue 1 na kuhitimisha ufalme wa mahasimu wao Paris Saint-Germain ambao wamekuwa wababe katika miaka ya hivi karibuni.
    REKODI

    AS Monaco imefunga mabao 103 katika michezo 37.

    Ubingwa:2017,2000,1997,1988,1982,1978,1963,1961.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: AS Monaco yatwaa ubingwa wa Ligue 1 baada ya miaka 17 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top