728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, May 30, 2017

    Vita ya Makala , Manara amjibu Edo kumwembe Simba sio Wavulana


    JICHO LA MWEWE AU LA KUKU??
    _______________________________________ Edo Kumwembe

    Na:HAJI Manara

    Kuna uchokozi flani unaofanywa na baadhi ya watu,haufai kunyamaziwa,hata kama unafanywa na mtu mnayejuana kitambo na mnayeheshimiana. 

    Nimesoma makala ya Eddo kumwembe mchana huu,nikajiuliza hili ni kweli jicho la Mwewe au sasa limekuwa la kuku?.

    Makala yake imejaa dharau na dhihaka kubwa kwa wachezaji wetu wa Simba,iliyojaa kebehi na ilioonyesha dharau kubwa iliopitiliza kwa watu ambao kivyovyote vile hawawezi kumjibu mchambuzi huyu. 

    Unapowadharau wachezaji hawa waliopigana kwa ajili ya klabu hii ni kutowatendea haki,na tukinyamaza tutakuwa MAJUHA. 



    Eddo rafiki yangu unapowaita wachezaji wetu ni wavulana na hawawezi kupambana kwenye mechi ngumu,na kuwaita wachezaji wa Yanga wanaume,,ulitumia kigezo kipi?hzi team kwa msimu huu zimekutana mara tatu,niseme wazi,hao wanaume tuliwafunga mara tatu tulizokutana. 

    Ndio mara zote Tatu!!game ya kwanza,wamshukuru mwamuzi Saanya,kwa kukataa goli letu la halali la MVULANA Ibrahim Ajibu,kisha kukubali goli la hovyo zaidi kufungwa kwa miaka kumi ilipita ktk ligi kuu ya Tanzania,goli la NETBOLI la MWANAMME TAMBWE,,kisha bila sababu yoyote akamtoa MVULANA Jonas Mkude kwa kadi nyekundu,usisahau WAVULANA unaosema hawawezi kupambana ktk mazingira magumu,walisawazisha goli wakiwa pungufu,kwa goli la kona la MVULANA kichuya,aliyetusahaulisha MWANAMME BARTHEZI. 

    Nikukumbushe pia,kule Zbar kwenye mapinduzi cup,hao.WANAUME tuliwafunga kwa penati,najua wajua WAVULANA waliingia fainali. 

    Kioja cha hao uliowanasibu ni WANAUME,tuliwadhalilisha feb 25,tukiwa pungufu tena kwa magoli ya kistadi toka kwa WAVULANA Kichuya na Mavugo,sijui unajua goli la Kichuya ndio goli bora msimu huu!! 

    Hv hapo huoni kuwa umewakosea kulikopitiliza WAVULANA?Nikusaidie mchambuzi wangu,game zote tatu Simba iliongoza kwa umilikaji mpira,hata zile tulizokuwa pungufu uwanjani,,sijui hapo nani MVULANA na nani MWANAMME?

    Kwa kuwa ww ni swahiba wangu,nikupe leo kwa faida yako na wasomaji wako,utofauti wa utanashati,uvulana na uliouita UBISHOO, Hawa wachezaji wa zama za leo,ni watanashati hata vwanjani,wanaweka style za nywele na hawanuki jasho la KUPUO,wanatoka jasho la kazi,kisha WAVULANA wa Simba unaowakusudia ww kina Ndemla,Ajibu,Mkude na Tshabalala,hawa hawajatoka MBWINDE,

    hawa ni born town,hawawezi kwenda uwanjani na nywele za fashion ya kizamani ya Denge,kama askari wa Mkoloni au Mgambo wa zone, MVULANA Mohd Husein Tshabalala ndio mchezaji bora ktk ligi kuu ya Vodacom na WANAUME hawakuipata tuzo hyo kubwa iliyokuja na mzigo wa BOKSI KUMI, ten M bro!!. 

    Nikujuze pia hili la kusema Method Mwanjale ni mzee ndio maana kachelewa kupona,,unasahau MVULANA Donald Ngoma nae hajapona hadi leo,kupona inategemea na namna ulivyoumia,ingekuwa kupona ni ujana pekee angepona Marco Van Basten,na asingerudi uwanjani Francesco Toti,mzee aliyestaafu juzi soka.

    Hoja ya kuwa Simba iliongoza kwa muda mrefu na kisha Yanga kutwaa ubingwa,Sijui rafiki yangu unakosea wapi!! kwanza Eddo nikuarifu na wasomaji wako, FIFA watarudisha points za Simba pasi na shaka yoyote ile,hakuna namna timu ichezeshe mchezaji mwenye kadi tatu za njano,kisha uinyime hyo timu ushindi,nikujuze pia ktk mpira hilo ni jambo la kawaida sana,Yanga waliwahi kuongoza ligi kwa points kumi na tano,baadae Simba wakaja kuwa mabingwa,huko Ulaya Madrid alikuwa anaongoza ligi kwa points nyingi lakini almanusura aukose ubingwa wa La liga msimu huu,,unakumbuka klabu yako unayoshabikia ya Arsenal tena ikiwa na WANAUME wa ukweli kina Patrick Viera,Sol Campbell ilikuwa ikiongoza ligi kwa points kumi na mbili,lakini mwishoe Mabishoo kina Beckam na klabu ya Manchester united wakachukua ndoo siku ya mwisho wa msimu wa EPL,wakati mwingine soka ipo hvyo, na kwa level na uelewa wako, sikutegemea uandike hoja za washabiki maandazi kama hizo.

    Nimekusoma pia ulivyosema kuwa Simba ilipata tabu kwa timu ndogo kama Mbao NK,

    hahahahaha,mchambuzi una utani na Gongowazi sio?? Mbao tumekutana nae mara tatu msimu huu na zote tumewafunga, au hujui?WANAUME KAPIGWA GAME MBILI NA MBAO MSIMU HUU, kama umejisahaulisha,habari ndio hyo!!
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Vita ya Makala , Manara amjibu Edo kumwembe Simba sio Wavulana Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top