728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, May 29, 2017

    Hatimaye Barcelona yampata mrithi wa Enrique


    Barcelona,Hispania.

    HATIMAYE Barcelona leo imemtangaza kocha wa zamani wa Athletic Bilbao,Ernesto Valverde kuwa Kocha wake mkuu mpya.

    Valverde,53,maarufu kama El Txingurri amekubali mkataba wa miaka miwili akichukua nafasi ya Luis Enrique aliyetangaza kujiweka pembeni baada ya kuhudumu kwa miaka mitatu.

    Kabla ya kujiunga na Athletic Bilbao,Valverde aliwahi kuvinoa vilabu vya Espanyol, Olympiacos, Villarreal pamoja na Valencia.

    Valverde aliwahi kuichezea Barcelona kwa kipindi cha miaka miwili kati ya 1988 na 1990.Wakati huo Barcelona ilikuwa ikinolewa na Mholanzi,Johan Cruyff.

    Valverde atatambulishwa mbele ya waandishi wa habari siku ya Alhamisi na kuwa kocha wa 56 wa Barcelona.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Hatimaye Barcelona yampata mrithi wa Enrique Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top