Barcelona, Hispania.
LIONEL Messi (Pichani) ametengeneza bao moja,amefunga mabao mawili na kuiwezesha Barcelona kuifunga Sevilla mabao 3-0 katika mchezo safi wa ligi ya La Liga ulioisha hivi punde huko dimbani Camp Nou jijini Barcelona.
Messi ambaye alikosa mchezo wa Jumamosi iliopita dhidi ya Granada kutokana na kutumikia adhabu ya kukosa mchezo mmoja ameandikisha mabao yake katika dakika za 28 na 33. huku lile Luis Suarez
Ushindi huo umeifanya Barcelona ifikishe pointi 69 na kukalia kwa muda kiti cha uongozi ligi ya La Liga kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya wapinzani Real Madrid wenye pointi 68
68 na michezo miwili mkononi.Baadae Real Madrid watashuka dimbani kucheza na Leganes na ikiwa watashinda mchezo huo wakarejea kileleni.
Sevilla ambao walilazimika kumaliza wa leo wakiwa wakiwa na wachezaji kumi (10) baada ya kiungo wake,MachÃn Pérez Vitolo kutolewa uwanjani kwa kadi mbili za njano wako nafasi ya nne wakiwa na pointi 58.
0 comments:
Post a Comment