728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, April 26, 2017

    Tunahitaji Pingu na Bastola Kumzuia Messi Usiku Wa Leo


    Barcelona, Hispania.

    KOCHA wa Osasuna,Petar Vasiljevic amesema kikosi chake kitahitaji msaada wa ziada leo usiku kuweza kumzuia Lionel Messi pale kitakaposhuka dimbani Camp Nou kucheza na Barcelona katika muendelezo wa michezo ya ligi ya La Liga.

    Vasiljevic ambaye juzi Jumapili alikuwa sehemu ya mashabiki waliomshuhudia Messi akifunga mabao mawili dhidi ya Real Madrid,Santiago Bernabeu amewataka wachezaji wake kutoonyesha uoga licha ya ukweli kwamba kichapo kutoka kwa Barcelona kitawafungulia rasmi milango ya kushuka daraja.

    Tayari nimeshasema kwamba tunahitaji mpango madhubuti kuweza kumzuia Messi leo.Wachezaji wangu wameniambia tunahitaji kubeba pingu pamoja na bastola ili kumzuia Messi.Amesema Vasiljevic.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Tunahitaji Pingu na Bastola Kumzuia Messi Usiku Wa Leo Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top