728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, April 26, 2017

    Ligi kuu England Leo:Michezo mitatu kupigwa leo,Arsenal,Spurs dimbani,Kesho Manchester Dabi,Ratiba yote ya wiki iko hapa

    London, England.

    BAADA ya jana Jumanne usiku kuishuhudia Chelsea ikiifumua Southampton mabao 4-2 nyumbani Stamford Bligde ligi kuu ya soka nchini England (Premier League) inatarajiwa kuendelea tena leo Jumatano kwa michezo mitatu kuchezwa katika viwanja vitatu tofauti huku timu sita zikitoleana makucha kuhakikisha zinajipatia alama tatu muhimu.

    Arsenal ambao wako kwenye hatari kubwa ya kushindwa kutinga nne bora msimu huu watakuwa nyumbani Emirates kuwaalika mabingwa watetezi wa ligi hiyo,Leceister City.

    Middlesbrough watakuwa nyumbani kwao Riverside kucheza na Sunderland na mchezo wa mwisho leo hii utakuwa kati ya Crystal Palace watakaokuwa nyumbani kwao Selhurts kuwaalika Tottenham.

    Ligi hiyo itaendelea tena kesho Alhamis kwa mchezo mmoja kuchezwa ambapo mahasimu wa jiji la Manchester,Manchester City watakuwa uwanjani kwao kupepetana na Manchester United.

    Ratika Kamili

    Jumatano Aprili 26,2017

    Arsenal v Leicester City (9:45 Usiku)
    Middlesbrough v Sunderland (9:45 Usiku)
    Crystal Palace v Tottenham (10:00 Usiku)

    Alhamis Aprili 27,2017

    Man City v Man Utd (10:00 Usiku)

    Jumamosi Aprili 29,2017

    Southampton v Hull City (11:00 Jioni)
    Stoke City v West Ham (11:00 Jioni)
    Sunderland v Bournemouth (11:00 Jioni)
    West Brom v Leicester City (11:00 Jioni)
    Crystal Palace v Burnley (1:30 Usiku)

    Jumapili Aprili 30,2017

    Man Utd v Swansea (8:00 Mchana)
    Everton v Chelsea (10:05 Jioni)
    Middlesbrough v Man City (10:05 Jioni)
    Tottenham v Arsenal (12:30 Jioni)


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Ligi kuu England Leo:Michezo mitatu kupigwa leo,Arsenal,Spurs dimbani,Kesho Manchester Dabi,Ratiba yote ya wiki iko hapa Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top