Lubumbashi, DR Congo.
TP Mazembe imeendelea vyema na kampeni zake za kuhakikisha kuwa inafuzu hatua ya makundi ya michuano ya kombe la shirikisho Afrika baada ya Jumapili jioni kuwatungua Waarabu wa Algeria,JS Kabylie kwa mabao 2-0 huko Lubumbashi.
Ikicheza kwenye dimba lake la Stade de Lubumbashi, TP Mazembe ilijipatia mabao yake kupitia kwa Mzambia,Nathan Sinkala na mlinzi wa Mali,Salif Coulibaly.
Timu hizo zitarudiana tena Jumapili ijayo huko Stade
du Tizi-Ouzou huko Algeria ambapo timu itakayopata ushindi mkubwa wa jumla itakuwa imefuzu hatua ya makundi ambayo inatarajiwa kuanza mwezi ujao.
Matokeo mengine ya michezo ya kombe la shirikisho Afrika.Club Africain ya Tunisia ikiwa ugenini Curepipe imechomoza na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Port Louis ya Mauritia.
Enugu Rangers ya Nigeria ikiwa nyumbani Enugu imelazimishwa sare ya mabao 2-2 na Zesco United ya Zambia.Tanda ya Ivory Coast imeifunga Platinum Stars ya Afrika Kusini mabao 2-0.
Matokeo Kamili
Port Louis (Mauritius) 1-2 Club Africain (Tunisia)
TP Mazembe (DR Congo, holders) 2-0 JS Kabylie (Algeria)
Enugu Rangers (Nigeria) 2-2 Zesco United (Zambia)
Tanda (Ivory Coast) 2-0 Platinum Stars (South Africa)
0 comments:
Post a Comment