Cairo,Misri.
WINGA wa zamani wa Mashetani Wekundu wa Manchester United,Ryan Giggs ameitaka klabu yake hiyo ya zamani kuiga mfano wa wapinzani wao Liverpool katika upachikaji mabao.
WINGA wa zamani wa Mashetani Wekundu wa Manchester United,Ryan Giggs ameitaka klabu yake hiyo ya zamani kuiga mfano wa wapinzani wao Liverpool katika upachikaji mabao.
Giggs ameyasema hayo akiwa
nchini Misri alipokwenda kwenye ziara ya kulitembeza kombe la klabu bingwa
Ulaya inayojulikana kama Heineken Champions League Trophy Tour.
Giggs ambaye kwa sasa anafanya kazi ya uchambuzi wa
masuala ya soka kwenye Televisheni za Uingereza ameitaka Manchester United kuacha
kumtegemea zaidi Zlatan Ibrahimovic katika upachikaji mabao na badala yake mabao yawe yanapatikana
kutoka pande zote za uwanja kama wafanyavyo Liverpool.Tofauti na hali ilivyo sasa,Ibrahimovic
akikosekana na mabao yanakosekana.
Nyota huyo raia wa Wales anapingana
na mashabiki wa klabu hiyo ambao wanaoamini kuwa kushindwa kufunga mabao ya
kutosha kwa Manchester United kunasababishwa na kukosa bahati pamoja na makosa
ya kizembe ya waamuzi wanaochezesha michezo ya klabu yao.
Mabao yanapaswa kupatikana
kutoka kila pande za uwanja.Hivyo ndiyo Manchester
United yetu ilivyokuwa.Ningefunga mabao saba au manane,Becks hivyo
hivyo,Scholes pia.Washambuliaji wote wanne wa mbele.Mabeki wa kati.Denis Irwin
pia.Mabao alipatikana kutoka kila pande za uwanja.
Huwezi kumtegemea mtu mmoja pekee kwa sababu anaweza akawa hayuko
fiti ama hayuko kabisa mchezoni.Leceister City msimu uliopita ilikuwa sawa.
Jamie Vardy alifunga mabao mengi na Riyad Mahrez akafunga 17.Hicho ndicho
unachohitaji.
0 comments:
Post a Comment