728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, April 08, 2017

    Baada ya Lingard kusaini mkataba mpya,hii ndiyo sura mpya ya mishahara Man United


    Manchester,England.

    JUZI Alhamisi staa wa England,Jesse Lingard alisaini mkataba mpya wa miaka minne wa kuendelea kusalia klabuni Manchester United.

    Lingard mwenye umri wa miaka 24 amezawadiwa  mkataba huo mnono utakaodumu mpaka mwaka 2021 baada ya kuonyesha kiwango bora katika misimu miwili iliyopita.Mkataba huo mpya umeripotiwa kuwa utakuwa ukimwingizia Lingard mshahara wa Paundi 100,000 kwa wiki.Mara tatu zaidi ya ule wa awali wa Pauni 30,000 kwa wiki.

    Mshahara huo mpya umemfanya Lingard aingie kwenye orodha ya nyota wanaovuta mkwanja mrefu zaidi klabuni Manchester United mbele ya mastaa kama Michael Carrick,Erick Bailly na Antony Martial.

    Ifuatayo ni orodha wa wachezaji wanaovuta mshahara mrefu zaidi kalabuni Manchester United

    1. Wayne Rooney: £300,000/w 
    2. Paul Pogba: £290,000/w 
    3. Zlatan Ibrahimovic: £220,000/w
    4. David De Gea: £200,000/w
    5. Henrikh Mkhitaryan: £180,000/w
    6. Juan Mata: £145,000/w
    7. Marouane Fellaini: £120,000/w
    8. Phil Jones: £120,000/w
    9. Chris Smalling: £120,000/w 
    10.Luke Shaw: £100,000/w
    11.Jesse Lingard: £100,000/w
    12.Michael Carrick: £80,000/w 
    13.Eric Bailly: £75,000/w
    14.Anthony Martial: £70,000/w
    15.Marcus Rashford: £35,000/w
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Baada ya Lingard kusaini mkataba mpya,hii ndiyo sura mpya ya mishahara Man United Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top