Basel, Uswisi.
SHIRIKISHO la vyama vya Soka Barani Ulaya (UEFA) limetangaza kikosi cha wachezaji 18 waliofanya vizuri zaidi katika michuano yake ya Europa Ligi iliyoisha hivi karibuni kwa Sevilla kutwaa ubingwa baada ya kuifunga Liverpool kwa mabao 3-1 huko St Jakob Park,Basel-Uswisi.
Katika kikosi hicho Mabingwa Sevilla wametoa wachezaji saba huku Ligi Kuu ya England ikifanikiwa kutoa wachezaji wanne pekee.Wachezaji hao ni David De Gea,Philippe Coutinho,Toby Alderweireld na Emre Can
Ujerumani imetoa wachezaji watatu,Hispania tisa na Ukraine wawili .
KIKOSI KAMILI
Makipa:David Soria (Sevilla)
David De Gea (Manchester United)
Mabeki:Toby Alderweireld (Tottenham Hotspur),Mats Hummels (Borussia Dortmund),Adil Rami (Sevilla),Mariano (Sevilla),Darijo Srna (Shakhtar Dontesk)
Viungo:Emre Can (Liverpool),Gonzalo Castro (Borussia Dortmund),Philippe Coutinho (Liverpool),Ever Banega (Sevilla),Grezegorz Krychowiak (Sevilla),Steven N’Zonzi (Sevilla),Marlos (Shakhtar Donetsk)
Washambuliaji:Aritz Aduriz (Athletic Bilbao),Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund),Cedric Bakambu (Villarreal) na Kevin Gameiro (Sevilla)
0 comments:
Post a Comment