Dar Es Salaam,Tanzania.
MABINGWA wa ligi kuu Tanzania bara,Yanga SC leo wameutumia vyema Uwanja wa Taifa,Dar Es Salaam baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya MC Alger ya Algeria katika mchezo wa kwanza wa hatua ya kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ya michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.
Bao pekee la mchezo huo limefungwa na kiungo wa kimataifa wa Zimbabwe,Thabani Kamusoka katika dakika ya 60 baada ya kazi nzuri ya Mnyarwanda,Haruna Niyonzima Fabregas.
Timu hizo zitarudiana tena Jumamosi ijayo huko Alger,Algeria na timu itakayopata ushindi mkubwa itafuzu hatua ya makundi.
Yanga SC leo iliwakilishwa na
1. Deogratius Munishi
2. Hassani Kessy
3. Haji Mwiji
4. Nadir Haroub
5. Vicent Bossou
6. Juma Saidi
7. Saimoni Msuva
8. Thabani Kamusoko
9. Obrey Chirwa
10. Haruna Niyonzima
11. Deusi Kaseke/Donald Ngoma
0 comments:
Post a Comment