Genk,Ubelgiji.
TIMU ya KRC Genk ya Mtanzania,Mbwana Samatta imeendelea kujisafishia njia ya kucheza michuano ya Europa Ligi msimu ujao baada ya usiku huu ikiwa ugenini huko Schiervelde kuwafunga wenyeji wao Roeselare kwa bao 1-0 katika mchezo mkali wa kundi A hatua ya mtoano.
Bao pekee la mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi,Nathan Verboomen limetiwa kimiani katika dakika ya 84 na José Manuel GarcÃa Naranjo.
Ushindi huo umeifanya KRC Genk iendelee kujitanua kileleni mwa kundi hilo baada ya kufikisha pointi sita.Hii ni baada ya kucheza michezo miwili.
0 comments:
Post a Comment