728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, June 07, 2016

    RASMI:UCHAGUZI YANGA SC JUNI 11,TFF YATOA GO AHEAD

    Dar es Salaam,Tanzania.

    Rais wa TFF Bw. Jamal Malinzi leo alikutana na secretariat ya Yanga chini
    ya Mwenyekiti anayemaliza muda wake madarakani Bw. Clement Sanga na
    Katibu Mkuu wa klabu hiyo Baraka Deusdedit kwa ajili ya kujadili mustakabali wa uchaguzi wa Yanga ambao uliingia katika mvutano na TFF pamoja na BMT.

    Maamuzi yaliyotoka ni kwamba,uchaguzi wa Yanga umebarikiwa kuendelea kama ulivyopangwa na kamati
    ya uchaguzi ya Yanga kwamba utafanyika June 11, 2016 chini ya uangalizi wa kamati ya uchaguzi ya TFF.

    Wagombea wa nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi huo ambao walichukua fomu TFF, kikao kimeamua kiwarudishe kamati ya uchaguzi ya Yanga kuendelea na taratibu zilizopo za uchaguzi endapo wanakidhi vigezo vya uchaguzi vya kamati ya uchaguzi ya Yanga.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RASMI:UCHAGUZI YANGA SC JUNI 11,TFF YATOA GO AHEAD Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top