728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, June 19, 2016

    LIGI YA MABINGWA AFRIKA:ZAMALEK YAVUNA USHINDI NYUMBANI KWA ENYIMBA

    Port Harcourt,Nigeria.

    ZAMALEK ikiwa ugenini nchini Nigeria imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Enyimba katika mchezo mkali wa Kundi A wa kombe la klabu bingwa Afrika uliochezwa jioni ya leo katika uwanja wa Adokiye Amiesimaka Stadium ulioko Port Harcourt,Nigeria.

    Bao pekee la mchezo huo limefungwa kwa kichwa dakika ya 8 na mshambuliaji hatari Bassem Morsy.

    Katika mchezo mwingine wa Kundi A uliochezwa jana Jumamosi Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ikiwa ugenini Algeria iliichapa ES Setif kwa mabao 2-0 ya Tiyiani Mabunda na Khama Billiat.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI YA MABINGWA AFRIKA:ZAMALEK YAVUNA USHINDI NYUMBANI KWA ENYIMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top