728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, June 09, 2016

    HODGSON: NGONO RUKSA EURO 2016

    Paris,Ufaransa.

    KOCHA wa timu ya taifa ya England,Three Lions Roy Hodgson ametangaza rasmi na kuwaambia wachezaji wake ngono ni ruksa kwa yeyote yule katika kipindi watakachokuwa katika Michuano ya Euro 2016.

    “Ninawaamini wachezaji wangu kuwa watafanya kilicho sahihi muda wote
    tunapokuwa uwanjani hata nje ya uwanja huwa wanafikiria michezo ya
    mbele,” alisema kocha huyo. 

    Kauli hiyo ya Hodgson inakinzana na ile iliyotolewa mwaka 2006 na Fabio Capello kwa wachezaji wa kikosi hicho katika fainali za kombe la dunia huko Ujerumani.Capello alikataza vikali ngono kwa wachezaji na kusema kuwa inachangia kuwadhoofisha wachezaji pindi wanapokuwa uwanjani.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: HODGSON: NGONO RUKSA EURO 2016 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top