728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, June 04, 2016

    CAMEROON YAWA NCHI YA TATU KUFUZU AFCON 2017

    Nouakchott,Mauritania.

    TIMU ya taifa ya Cameroon imekuwa nchi ya tatu kufuzu Fainali za Kombe
    la Mataifa ya Afrika AFCON 2017 baada ya Ijumaa usiku kupata ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya Mauritania katika mchezo mkali wa kufuzu wa kundi M huko Nouakchott,Mauritania.

    Bao lililoipeleka Cameroon katika fainali hizo zitakazopigwa huko Gabon mwakani limefungwa kwa mkwaju dakika ya 29 na kiungo wake Edgar Salli.

    Kwa ushindi huo Cameroon sasa wanaungana na mataifa ya Algeria, Morocco na wenyeji Gabon kujihakikishianafasi ya kucheza AFCON  mwakani.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CAMEROON YAWA NCHI YA TATU KUFUZU AFCON 2017 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top