728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, August 15, 2015

    TETESI ZA USAJILI JUMAMOSI:MANGALA,OTAMENDI KUPISHANA MLANGONI ETIHAD,MADRID YATENGA MTONYO MKUBWA KUMSAJILI WILLIAM CARVALHO

    Carvalho:Real Madrid inaandaa kitita cha €45m ili kumsajili kiungo mahiri wa Sporting ya Ureno William Carvalho,21.Real Madrid imezidisha kasi baada ya Sporting Lisbon kumsajili Muitaliano Alberto Aquilani.

    Otamendi:Manchester City iko tayari kutoa kitita cha pesa pamoja na mlinzi wake Eliaquim Mangala ili kumsajili mlinzi wa Valencia Nicolas Otamendi. (Daily Mirror)

    Berahino:Baada ya kumuuza mshambuliaji wake Roberto Soldado kwenda Villarreal Tottenham inaandaa kitita cha £15m kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa West Brom Saido Berahino,21.Hata hivyo mpango huo huenda ukakwama kwani West Brom imeendelea kusisitiza haitamwachia nyota huyo kwa dau la chini ya £25m.(Daily Telegraph)

    Burak:West Ham imeendelea kusaka mshambuliaji mpya na safari hii jicho lake limetua kwa mshambuliaji wa Galatasaray Burak Yilmaz,30.West Ham imeandaa kitita cha €10 ili kumnasa mkali huyo wa mabao tuko Uturuki.(Metro)

    Destro:Norwich City ina matumaini makubwa ya kuipiku Bologna katika mbio za kuinasa saini ya mshambuliaji wa AS Roma Mattia Destro,24. (Norwich Evening News)

    Illarramendi:Liverpool iko katika nafasi nzuri ya kumsajili kiungo Asier Illarramendi,25 baada ya Real Madrid kuwa tayari kumuuza nyota huyo wa zamani wa Real Sociedad.(Metro)



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TETESI ZA USAJILI JUMAMOSI:MANGALA,OTAMENDI KUPISHANA MLANGONI ETIHAD,MADRID YATENGA MTONYO MKUBWA KUMSAJILI WILLIAM CARVALHO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top