728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, August 19, 2015

    MARADONA AKUTANA NA REFA ALIYELIKUBALI GOLI LAKE LA MKONO LA MWAKA 86,ALICHOMFANYIA HAWEZI KUSAHAU








     Unaikumbuka fainali ya kombe la dunia la mwaka 1986?Unalikumbuka goli la mkono wa Mungu aliliolifunga Maradona katika mchezo wa robo fainali dhidi ya England katika dimba la Azteca?Unamkumbuka mwamuzi aliyechezesha mpambano ule?Kama umesahau anaitwa Ali Bennaceur raia wa Tunisia.

    Sasa mapema wiki hii wawili hao walikutana jijini Tunis ambapo Maradona alikwenda kutengeneza tangazo la biashara.Baada ya Maradona kumuona Ali alimfuata akamkumbatia na kumpiga mabusu yasiyo na idadi na kisha kumkabidhi jezi ya Argentina ikiwa na saini yake pamoja na maandishi yaliyosomeka "Ali rafiki yangu wa ndani"
     Diego Maradona kissed and hugged the referee who allowed his infamous hand of God goal in the 1986 World Cup after meeting him on a trip to Tunisia
    Ali,hakuzubaa nae akajibu mapigo kwa kumpa Maradona picha inayomuonyesha yeye (Ali),Maradona na mlinda mlango wa England siku ile Shilton,waliyopiga pamoja katika dimba Azteca Stadium,Mexico kabla ya kuanza kwa mchezo ule.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MARADONA AKUTANA NA REFA ALIYELIKUBALI GOLI LAKE LA MKONO LA MWAKA 86,ALICHOMFANYIA HAWEZI KUSAHAU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top