728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, August 29, 2015

    U-TURN:SIMBA YAPIGA CHINI WASENEGAL YAMRUDISHA MRUNDI NDAYISENGA

    Uongozi wa klabu ya Simba
    umeamua kuchana na Wasenegali wote na sasa inamrudisha Kelvin Ndayisenga.

    Ndayisenga raia wa Burundi
    alifanya majaribio Simba akafuzu lakini ikawa tatizo katika suala la
    makubaliano ya kifedha.Pamoja na kutaka dau la zaidi ya Sh milioni 80,Ndayisenga alitaka alipwe Sh 200,000 kwa kila bao atakalofunga.

    Simba ikaamua kuachana
    naye na kumleta Papa Niang
    kutoka Senegal ambaye alishindwa kuonyesha uwezo.

    Aliposhindwa, ikamshusha Abdoulaye Nd’aw ambaye pia alionyesha hana lolote baada ya kuanguka mazoezini akionekana hayuko fiti.

    Taarifa zinaendeleza Ndayisenga anarejea Dar es Salaam kujiunga na Simba baada ya Simba kukubaliana na wakala wake, Denis Kadito, Mtanzania anayeishi nchini Uholanzi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: U-TURN:SIMBA YAPIGA CHINI WASENEGAL YAMRUDISHA MRUNDI NDAYISENGA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top