728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 06, 2016

    BORUSSIA DORTMUND YAJIBU MAPIGO YACHOMOA MMOJA BAYERN MUNICH

    Dortmund, Ujerumani.

    Baada ya kupokwa wachezaji wake kwa kipindi kirefu Borussia Dortmund hatimaye leo imejibu mapigo baada ya kufanikiwa kumsajili kiungo Mjerumani Sebastian Rode toka Bayern Munich kwa ada ambayo haijawekwa wazi.

    Rode,25,amesaini mkataba wa miaka minne wa kuichezea miamba hiyo ya Signal Iduna Park baada ya kufuzu vipimo vya afya jioni ya leo. 

    Kabla ya kutua Bayern Munich,Rode aliichezea Eintracht Frankfurt.Mpaka anaiacha Bayern Munich Rode amefanikiwa kuanza michezo 11 katika kipindi cha misimu miwili aliyokaa Allianz Arena.

    Rode anakuwa mchezaji wa nne kujiunga na Borussia Dortmund.Wengine ni Marc Bartra,Ousmane Dembele na Mikel Merino.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BORUSSIA DORTMUND YAJIBU MAPIGO YACHOMOA MMOJA BAYERN MUNICH Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top