728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, June 15, 2016

    MZIMBABWE ASAINI MIAKA MIWILI JANGWANI

    Dar es Salaam,Tanzania.

    KATIKA kuhakikisha inaimarisha safu yake ya ushambuliaji, uongozi wa klabu ya Yanga umefanikiwa kumalizana na straika kutoka FC Platinum ya Zimbambwe, Walter Musona, baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili.

    Walter ni mchezaji aliyependekezwa na kiungo na straika wa timu hiyo, Thabani Kamusoko na Donald Ngoma ambao wamecheza naye muda mrefu wakijua uwezo wake ndani ya uwanja.

    Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Yanga, zinadai kwamba straika huyo alitakiwa kuwasili wiki mbili zilizopita ikashindikana lakini sasa mambo yanakwenda sawa.

    Kuchelewa huko kulitokana na Yanga kutafuta njia nzuri za kuachana na Mniger Boubakar Issouf, ambaye ameshindwa kuendana na kasi ya Wanajangwani hao lakini sasa taarifa zinadai kuwa kila kitu kimekwenda sawa.

    “Sasa kila kitu kinaenda vizuri baada ya kumaliza mchakato wa kulipwa haki zake Mniger pamoja na uchanguzi, Musona anatua wakati wowote na kusaini mkataba wa miaka miwili,” alisema kigogo mmoja kutoka Yanga.

    Kigogo huyo alisema baada ya kusaini mkataba ataungana na wachezaji wenzake nchini Uturuki kwa ajili ya kambi kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Mo Bejaia ya Algeria.

    Wakati huo huo Mkuu wa Idara ya habari na Mawasiliano, Jerry Muro, alithibitisha kuwepo kwa mazungumzo na mchezaji huyo na kuwahakikishia Wanayanga kuwa angetua nchini muda wowote.

    CHANZO:DIMBA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MZIMBABWE ASAINI MIAKA MIWILI JANGWANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top