728x90 AdSpace

Wednesday, November 25, 2015

PSG YAMFUNGIA KAZI RONALDO,YAMUANDALIA MSHAHARA AMBAO AKIUKATAA DUNIA ITAMSHANGAA

Paris,Ufaransa.

Cristiano Ronaldo huenda akaweka historia ya kuwa mwanasoka wa kwanza kulipwa mshahara wa £500 milioni kwa wiki ikiwa atakubali kujiunga na PSG mwishoni mwa msimu huu.

Taarifa kutoka nchini Ufaransa zinasema kuwa PSG imemtengea Ronaldo,30 ofa ya £250,000 kama mshahara wake wa wiki hii ni baada ya kukatwa kodi.[Sawa na £500,000 kabla ya kukatwa kodi] ili kuzima ndoto za nyota huyo Mreno kurejea katika klabu yake ya zamani ya Manchester United.

PSG kupitia kwa Rais wake Nasser Al-Khelaifi inamuona Ronaldo kama mrithi sahihi wa nyota wake Zlatan Ibrahimovic ambaye anatarajiwa kuachana na klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu pindi mkataba wake utakapikuwa umefikia tamati.

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: PSG YAMFUNGIA KAZI RONALDO,YAMUANDALIA MSHAHARA AMBAO AKIUKATAA DUNIA ITAMSHANGAA Rating: 5 Reviewed By: Unknown