728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, November 23, 2015

    PIGO ARSENAL:COQUELIN NJE YA DIMBA HADI MWAKANI,SASA MATUMAINI KWA FLAMINI


    London,England.

    Arsenal imepata pigo baada ya kiungo wake mkabaji Francis Coquelin kuripotiwa kuwa atakuwa nje kwa kipindi cha kati ya miezi mitatu au minne baada ya kuumia goti lake la mguu wa kulia. 

    Coquelin,24 alipata jeraha hilo siku ya jumamosi baada ya kugongana na kiungo wa West Bromwich Albion Claudio Jacob wakati wakigombea mpira katika mchezo ambao Arsenal ililala kwa mabao 2-1 na kushindwa kukaa kileleni mwa ligi kuu ya EPL.

    Kufuatia habari hiyo mbaya Arsenal italazamika kumtegemea Mathieu Flamini pekee baada ya kiungo mwingine Mikel Arteta naye kuwa majeruhi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PIGO ARSENAL:COQUELIN NJE YA DIMBA HADI MWAKANI,SASA MATUMAINI KWA FLAMINI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top